Kocha mkuu wa Yanga, Hans            van der Plujim (kulia)
        RUVU Sootings na Yanga            zitachuana kesho katika mechi ya ligi kuu soka Tanzania bara            itayopigwa uwanja wa Taifa Dar es salaam.
        Mechi ya raundi ya kwanza            iliyopigwa januari 17 mwaka huu uwanja wa Taifa, timu hizo            zilitoka suluhu (0-0).
        Hiyo ndio mechi pekee            ambayo Ruvu Shooting hawakuruhusu goli katika mechi 9            walizokutana kwa mwaka wa tano sasa (kuanzia 2010).
        Kipigo kikubwa zaidi Ruvu            Shootings kupokea kutoka kwa Yanga ni magoli 7-0 msimu            uliopita.
        kocha mkuu wa Yanga sc,            Hans van der Pluijm amewaongoza vijana wake katika mazoezi            yaliyofanyika asubuhi ya leo uwanja wa Karume Dar es salaam na            amesema: "Tuko tayari kwa mechi, tunajua kila mechi ni ngumu            kwetu, unapohitaji kuwa bingwa unahitaji kushinda kila mechi            iliyopo mbele yako. Tuko tayari kushinda ili tubakishe pointi            tatu za kutupa ubingwa".
        "Cannavaro (Nadir Haroub)            hayupo fiti kucheza kesho, siku zote siongelei wachezaji            wasiokuwepo kwenye programu yangu. Yanga ina  wachezaji zaidi            ya 25 na wate wanaweza kutumika".
        Yanga inaongoza ligi kuu            ikijikusanyia pointi 49 baada ya kushuka dimbani mara 22,            ikifuatiwa na Azam fc yenye pointi 42 katika nafasi pili baada            ya kucheza mechi 22.
        
Comments
Post a Comment