Newcastle imefungwa mechi ya sita mfululizo kwenye Premier League baada ya kukubali kipigo cha 3-1 kutoka kwa Tottenham.
Mashabiki wa klabu hiyo wameanza kuingiwa na mashaka ya kushuka daraja na haikushangaza pale baadhi ya0 walipobeba mabango ya kumtaka mmiliki wa timu Mike Ashley abwage manyanga.
Nacer Chadli aliifungia Tottenham bao la kwanza dakika ya 30 lakini Jack Colback akawasawazishia wenyeji muda mfupi baada ya mapumziko.
Christian Eriksen akawapa wageni bao la pili kwa free-kick tamu kunako dakika ya 53.
Dakika ya 90 mshambuliaji hatari wa Tottenham Harry Kane akafunga goli la tatu, hili likiwa bao lake la 30 kwa timu hiyo katika mashindano yote msimu huu.
NEWCASTLE (4-1-4-1): Krul 4; Janmaat 6.5, Williamson 6, Coloccini 6, Anita 6 (Armstrong 75, 6); R Taylor 6; Gouffran 4.5 (Ameobi 46, 6), Colback 6.5, Abeid 4.5 (Obertan 46, 6), Cabella 5.5; Perez 6.5.
TOTTENHAM (4-2-3-1): Vorm 6; Dier 6, Vertonghen 7, Fazio 6, Rose 6.5 (Davies 81); Paulinho 6.5 (Mason 88), Bentaleb 6.5; Lamela 6, Chadli 7.5 (Dembele 78), Eriksen 7; Kane 6.5.
Comments
Post a Comment