KOCHA mkuu wa Yanga, Hans            van der Pluijm amesema sasa malengo yake ni kushinda mechi            mbili zijazo ili kutwaa kombe lake la Kwanza Tanzania.
        Pluijm anayewakosa            wachezaji muhimu kwasasa kutokana na majeruhi wakiwemo Nadir            Haroub 'Cannavaro', Kelvin Yondan, Salum Telela amesema yeye            hazungumzii wachezaji majeruhi bali anazungumzia wachezaji            waliopo.
        "Timu hii inawachezaji            wengi, wote ni wazuri na unaweza kuwatumia wakati wowote. Leo            (jana) nimewakosa Cannavaro, Yondan, Telela, lakini Saidi            (Juma), Zahir (Rajabu), Mbuyu (Twite) wameziba mapengo hayo na            kupata ushindi". Amesema Pluijm.
        Kuhusu kumuweka benchi            goli kipa Ali Mustafa 'Bartez', Pluijm amesema yeye hana            wasiwasi na uwezo wa makipa wake.
        "Naamini Yanga ina makipa            wazuri, 'Dida (Deo Munishi) na kipa mzuri sawa na Bartez (Ali            Mustafa), kutokana na ubora wao nimeamua leo nimpumzishe            Bartez ili Dida acheze. Ni sababu za kimpira tu wala hakuna            kingine"  Amesema Pluijm.
        Kuhusu Andrey Coutinho            Pluijm amesema: "Kwa muda mrefu amekaa nje ya uwanja kutokana            na majeruhi, lakini sasa ameimarika ingawa si kwa asilimia            100, kicuhezaji anahitaji mechi angalau mbili zao ili kurudi            kwenye kiwango chake".
        
Comments
Post a Comment