Kiungo wa Manchester City, Yaya Toure            ameripotiwa kukubaliana suala la malipo binafsi na klabu ya            Inter Milan ya Italia kuelekea kukamilisha dili la uhamisho            wenye thamani ya pauni milioni 5.7 kiangazi hiki.
        Baada ya kiwango chake kuporomoka,            mustakabali wa Toure ndani ya Etihad umekuwa na shaka wakati            City ikionekana kutaka kukikwamua kikosi kwa kuwaacha            wachezaji wenye umri mkubwa na kujaza vijana wa Kiingereza            wenye kipaji.
        Uwepo wa Roberto Mancini katika klabu ya            Inter unaelezwa kuweka uwezekano mkubwa wa staa huyo wa            kimataifa wa Ivory Coast kuondoka City, na kwa mujibu wa            Sportsmediaset tayari amekubali mkataba wa miaka minne wenye            thamani ya karibu pauni milioni 12.8 ili kuichezea klabu hiyo            ya Serie A.
        Inter imeripotiwa kuilipa City pauni            milioni 5.7 na bonasi kwa ajili ya kiungo huyo mwenye umri wa            miaka 31 kama ataisaidia kupata tiketi ya kucheza Champions            League msimu ujao.
        
Comments
Post a Comment