MASHABIKI wenye bahati katika mji wa Ufaransa wa Saint-Etienne jana usiku walimuona Mbrazil Ronaldo na Zinedine Zidane wakicheza kwenye mechi ya 12 ya hisani ya mwisho wa mwaka kupinga umasikini.
Magwiji hao wa soka Ronaldo na Zidane waliungana na wenyeji wao, wachezaji wakubwa wa zamani wakiwemo Clarence Seedorf, Fabian Barthez, Jay-Jay Okocha na Gianluca Zambrotta.
Ronaldo amekuwa akisemekana kuwa na mpango wa kustaafu soka katika klabu yake ya Amerika ya Fort Lauderdale na nyota huyo mwenye miaka 38 jana alionesha kwamba bado ana vitu vitamu baada ya kufunga magoli matatu "hat trick'.
Nyota wa zamani wa Ufaransa, Zinedine Zidane alionesha kwamba bado yumo na hapa alikuwa anachuana na Torpe Svarme
Gwiji wa Brazil Ronaldo akigusa mpira kiufundi kutengeneza mashambulizi
Magwiji wakubwa wawili wa soka Ronaldo na Zidane wakipeana tano kwenye uwanja wa Geoffroy Guichard
Comments
Post a Comment