LIVERPOOL KUPITISHA PANGA KALI, WACHEZAJI 10 KWENDA NA MAJI …wamo Balotelli, Glen Johnson, Kolo Toure, Lambert na Fabio Borini
LIVERPOOL inaelezwa            itapitisha panga kufyeka wachezaji wake 10 kiangazi hiki            wakati Brendan Rodgers akitaka kusuka upya kikosi chake baada            ya kuhakikishiwa kubaki.
        The Reds imeshindwa            kuendeleza makali yake ya msimu uliopita ilipokuwa ikipigania            taji la Premier League na kwa sasa inashika nafasi ya tano,            ikiachwa pointi saba nyuma ya mstari wa tiketi ya Champions            League.
        Liverpool ililazimika            kutumia fedha nyingi baada ya Kombe la Dunia kufuatia kuondoka            kwa Luis Suarez aliyekwenda Barcelona, lakini wakali kama            Mario Balotell na Rickie Lambert wameshindwa kukidhi haja.
        Gazeti la Daily Mail            limedai nyota 10 watakaoondoka mwisho wa msimu ni pamoja na            Steven Gerrard ambaye tayari amethibitishwa kuhamia LA Galaxy            ya Marekani.
        Glen Johnson na Kolo            Toure wanatarajiwa kuwa huru baada ya mikataba yao kufika            mwisho, wakati Javi Manquillo hatapewa mkataba wa kudumu baada            ya kucheza kwa mkopo.
        Washambuliaji            Balotelli, Lambert na Fabio Borini wanatajwa kufunguliwa            mlango wa kutoka Anfield sambamba na Brad Jones, huku Martin            Skrtel ambaye hajasaini mkataba mpya akiwa na uwezekano wa            kuuzwa Wolfsburg, wakati Raheem Sterling akifukuziwa na            Manchester City, Chelsea na Arsenal.
        
Comments
Post a Comment