Kama hujui kwanini Ngassa alishangilia goli kwa kubusu mkono, sababu hii hapa!


Kama hujui kwanini Ngassa alishangilia goli kwa kubusu mkono, sababu hii hapa!
20150421_182508
YANGA SC imeshinda magoli 3-2 dhidi ya Stand United katika mechi ya ligi kuu iliyopigwa jana uwanja wa Taifa, Dar es salaam.
Magoli ya Yanga yalifungwa na Amissi Tambwe, Mrisho Ngassa na Saimon Msuva kwa mkwaju wa penalti.
Baada ya kufunga goli lake, Mrisho Ngassa hakushangilia kwa kawaida yake ya kwenda kwenye kona ya kibendera, bali alionekana akibusu mkono wake.
Mtandao huu ukadadisi, kwanini Ngassa anabusu mkono wake na kuamua kumuuliza baada ya mechi ana akajibu:
"Nimebusu mkono kwasabababu nimemchora 'Tattoo' mke wangu, mke wangu ndio kila kitu, ndio mshauri wangu wa kila kitu, kwahiyo nikifunga goli lazima nimbusu"
Tattoo niliyochora ni jina la mke wangu kwasababu nina mapenzo ya dhati kwake, yeye ndiye mshauri wangu, anaitwa Nish Radhia"
"Kuna tattoo nyingine ambayo ni siri yangu pamoja na yeye, imechorwa kifuani"


Comments