EDINSON CAVANI KUWASILISHA OMBI LA KUTAKA KUONDOKA PSG …akerwa kuchezeshwa kama winga, Man United yakaa mkao wa kula
Manchester United imepata matumaini            makubwa ya kushinda mbio za uhamisho wa pauni milioni 55 kwa            Edinson Cavani baada ya vyanzo vya habari vilivyo karibu na            staa huyo kusema atawasilisha hoja ya kutaka kuondoka kiangazi            hiki.
        Red Devils iko sokoni kusaka mshambuliaji            wakati ikijiandaa kuwatema Robin van Persie na Radamel Falcao            na bila shaka itafarijika kusikia nia ya Cavani kutaka            kuondoka Paris Saint-Germian.
        Chanzo kimoja kimeliambia gazeti la Le            Parisien la Ufaransa kwamba Cavani hatabaki kwa msimu mwingine            PSG kama upangaji kikosi hautabadilika.
        "Cavani amekuwa akipangwa kushambulia            kutokea upande wa kulia kwa miaka miwili sasa, lakini si            nafasi inayomfaa – anataka kuchezeshwa kama mshambuliaji wa            kati, nafasi anayopendelea na si hadi asipokuwapo            Ibrahimovic," kilisema chanzo hicho.
        Kilisema Cavani anataka kuendelea kupangwa            kama mshambuliaji wa kati ili kuonyesha ubora wake uliomfanya            kuwa kinara wa mabao Italia.
Louis van Gaal ana nia ya kumsainisha mshambuliaji huyo, lakini anakibiliana na ushindani kutoka Arsenal na Liverpool.
        Louis van Gaal ana nia ya kumsainisha mshambuliaji huyo, lakini anakibiliana na ushindani kutoka Arsenal na Liverpool.

Comments
Post a Comment