CAVANI SASA NDIYO HABARI YA MUJINI …PSG kuipiga tik tak Manchester United, Paul Pobga ahusishwa


CAVANI SASA NDIYO HABARI YA MUJINI …PSG kuipiga tik tak Manchester United, Paul Pobga ahusishwa

Taarifa mpya kutoka katika vyanzo vya habari nchini Italia na Ufaransa ni juu ya wawakilishi wa mshambuliaji wa kimataifa wa Uruguay, Edinson Cavani kukutana na menejimenti ya Paris Saint-Germain.
Kwamba lengo la mkutano huo ni kujadili ofa kutoka Juventus, Manchester United na Atletico Madrid zinazotaka huduma ya staa huyo wa zamani wa Napoli mwenye umri wa miaka 28.
Habari zaidi zinapasha kuwa kama PSG itaamua kumwachia Cavani kuondoka, basi atakwenda Juventus ili kuirahisishia klabu hiyo ya Ufaransa kupata saini ya Paul Pogba.


Comments