Jose            Mourinho ameanzisha tena vita ya maneno na Arsenal akisema            kukaa miaka 11 bila kombe ndiko 'kunaboa".
        John            Terry akiwa kwenye kiwango cha juu zaidi kuwahi kutokea, kwa            mujibu wa Mourinho aliiongoza Chelsea kupata suluhu Emirates            na kuukaribia ubingwa wa ligi kuu England.
        Mashabiki            wa Arsena walikuwa wanawazomea Chelsea kwa staili yao ya            kujihami wakidai inaboa.: 'Boring, boring".
        Mawazo            ya mashabiki yaliendana na Arsene Wenger aliyedai Chelsea            walienda Emirates kujilinda tu na si kucheza mpira, lakini            Mourinho aliyeanza mechi bila kuwa na mshambuliaji wa kati wa            wazi amejibu mapigo akisema kitendo cha Arsenal kukaa miaka 11            bila ubingwa wa ligi kuu ndiko kunaboa.
        "Inaboa,            nadhani ni miaka 10 bila ubingwa. Hii inaboa" amesema Mreno            huyo.
        "Unaishangilia            timu na unasubiri, unasubiri, unasubiri kwa miaka mingi bila            kombe, huko ndiko kunaboa"
        
Comments
Post a Comment