Arsenal imepata msukumo mkubwa katika            harakati zake za kukamilisha uhamisho wa kushtua wa kipa wa            Real Madrid, Iker Casillas baada ya kubainika kuwa miamba hiyo            ya Hispania inajaribu kumshawishi aondoke Santiago Bernabeu.
        Gunners ina nia ya kumsajili kipa huyo            mkongwe mwenye umri wa miaka 33 na inaweza kutimiza lengo            iwapo Mhispania huyo atatangaza kuondoka Madrid.
        Casillas ana mkataba hadi 2017 na kwamba            anataka heshima katika klabu yake, lakini kwa mujibu wa kituo            cha redio cha Onda Cero, Madrid iko tayari kumlipa ili aondoke            na kujiunga na Arsenal au Liverpool.
        Arsene Wenger anafuatilia kwa karibu hali            ya mambo inavyokwenda Madrid.
        
Comments
Post a Comment