ARSENAL KUWEKA MEZANI PAUNI MIL 10 KWA BEKI MATTEO DARMIAN WA TORINO YA ITALIA


ARSENAL KUWEKA MEZANI PAUNI MIL 10 KWA BEKI MATTEO DARMIAN WA TORINO YA ITALIA

Arsenal imejipanga kulipa pauni milioni 10.7 kwa ajili ya uhamisho wa beki anayepanda wa klabu ya Torino ya Italia, Matteo Darmian.
Kwa mujibu wa gazeti la Forza, staa huyo wa zamani wa Palermo mwenye umri wa miaka 25 aliitamanisha zaidi Arsenal baada ya kufunga bao moja na kupika jingine katika ushindi wa 2-1 dhidi ya Juventus.
Hata hivyo, Arsene Wenger anakabiliwa na upinzani kutoka kwa miamba ya Ulaya, Barcelona na Bayern Munich ambazo pia zinatamani huduma ya beki huyo aliyepanda thamani kutokana na kiwango chake bora msimu huu.


Comments