Tanzania            imepangwa kucheza na Uganda katika
          mechi ya ufunguzi ya michuano ya Afrika Ligi
          Daraja la kwanza itakayofanyika nchini Afrika ya
          Kusini katika mji wa Benoni mwishoni mwa wiki
          hii.
Chama cha Kriketi            nchini Tanzania kimeteua
          timu ya taifa kwa ajili ya michuano hiyo na tayari
          timu hiyo imeondoka Tanzania kuelekea Afrika
          ya Kusini.
Nahodha wa            Tanzania, Hamisi Abdallah
          amesema Uganda sio timu ngeni na
          wanaichukulia mechi yao kwa umuhimu
          mkubwa.Nchi nyingine zinazotegemewa kushiriki
          michuano hiyo ni Kenya, Namibia, Botswana na
          Ghana.
Abdallah            anaendelea kuwa nahodha wa timu hiyo
          kwa zaidi ya muongo mmoja (miaka 10) akiwa
          na uzoefu wa kutosha wa michuano ya
          kimataifa, huku akiwa na rekodi ya kucheza
          kriketi nchini Uingereza katika klabu ya Watford
          Town.
Wachezaji wengine            waliochaguliwa katika timu
          hiyo ni Abhik Patwa, akiwa na rekodi ya kufunga
          nusu century ( runs 50) katika michuano iliyopita
          ambapo Nigeria na Ghana waliibuka vinara.
Wachezaji wengine            ni Yakesh Patel, Ally Mpeka,
          Arshan Jassani, Riziki Kiseto, Zamoyoni
          Jabeneke,Harsheed Chohan, Issa Kikasi,Kassim
          Nassoro, Arun Dagar, Khalil Rehemtullah, Martin
          Mwarabu na Rahil Amarshi.
Comments
Post a Comment