Hart              akibasamu mbele ya Lionel Messi
        PAUL            Scholes amemkosoa Joe Hart kwa kitendo chake cha kufurahia            licha ya Manchester City kutolewa na Barcelona katika michuano            ya ligi ya mabingwa ulaya.
        Hart            alikuwa kwenye kiwango cha juu Nou Camp siku ya jumatato wiki            hii kwa kuokoa michomo mingi na kuifanya Barca asivuna magoli            mengi.
        Barcelona            walishinda mechi ya pili, shukuruni kwa bao pekee la kipindi            cha kwanza la Ivan Rakitic na Wakatalunya hao walisonga kwa            tofauti ya magoli 3-1.
        Hart aliokoa michomo mingi na              kuzuia magoli mengi  Nou Camp
        Akiandika            katika kolamu yake ya gazeti la  Independent, Scholes alisema: "Kazi            nzuri Joe Hart kwa kufanya kazi kubwa ya kuokoa michomo mikali            msimu huu ligi ya mabingwa, na bila yeye mambo yangekuwa            mabaya zaidi kwa City".
        "Lakini            kitu kimoja kisichoniingia kichwani ni ushahidi wa yeye            kufurahia. Baada ya mechi kumalizika alifurahia kila alipookoa            na kuwashangilia na mabeki wake.
        "City            walikuwa wanapoteza 1-0. Walikuwa wanatupwa nje ya ligi ya            mabingwa. Walikuwa wanashangilia nini? kupoteza 5-0?
        
Comments
Post a Comment