Kipa wa Bayern Munich Pepe Reina amesema David de Gea ni mmoja wa makipa bora barani Ulaya na hapo hapo kumtaka mlinda mlango huyo kubakia Manchester United licha kuwaniwa na Real Madrid.
De Gea ambaye alijiunga na United mwaka 2012 akitokea Atletico Madrid, alisota kuzoea maisha ya Premier League lakini sasa ni moja ya 'silaha' muhimu za Louis van Gaal msimu huu.
Kiwango chake kwa misimu miwili iyopita kilikuwa bora huku akiokoa michomo ya hatari katika namna ya kushangaza na sasa Real Madrid inaamini De Gea ndiye mtu sahihi wa kumrithi kipa Iker Casillas.
Lakini Reina, nyota wa zamani wa Liverpool amesema De Gea anatakiwa aachane kabisa na mpango wa Real Madrid.
"Ni mmoja wa makipa bora Ulaya na 'fomu' yake msimu huu ni ya hali ya juu, Reina aliiambia talkSPORT.
"Pengine Real Madrid inasaka kipa mpya na De Gea ni moja ya majina yanayotajwa, lakini nadhani atakuwa na furaha zaidi kwa kuichezea Man United."
Comments
Post a Comment