Mapumziko: Yanga waongoza 2-1 dhidi ya Kagera Taifa


Mapumziko: Yanga waongoza 2-1 dhidi ya Kagera Taifa

KAGERAMtanange wa ligi kuu ya Tanzania bara kati ya Dar es Salaam Young Africans pamoja na Kagera Sugar umemalizika kwa kipindi cha kwanza (Dk 45) Yanga wakiwa mbele kwa bao 2-1 kunako Uwanja wa Taifa.

Mabao ya Yanga yamefungwa na Simon Msuva katika dakika ya 7 kwa mkwaju wa penati pamoja na Amis Tambwe kunako dakika ya 14 kufatia pasi ya Mrisho Ngassa.

Bao la kagera Sugar limepachikwa na Salum Kanoni kwa mkwaju wa penati dakika ya 39.



Comments