LIONEL MESSI MWANASOKA TAJIRI ZAIDI DUNIANI, RONALDO WA PILI ….Van Persie kijogoo Premier League



Lionel Messi tops the France Football rich list for              2014 with an annual income of £47.8m 

Lionel  Messi ndiye mwanasoka anayelipwa zaidi duniani, akiwa anaingiza karibu pauni milioni 1 kwa wiki kupitia mshahara pamoja dili za wadhamini.

Nyota huyo wa Argentina na Barcelona ameweka kibindoni pauni milioni 47.8 kwa mwaka 2014 ndani yake ikiwa ni mshahara wa pauni milioni 26 ukijaziwa na malipo ya kutoka kwa wadhamini adidas, FIFA 15 na Turkish Airlines.

Hiyo inamweka Messi mbali kabisa na mpinzani wake mkubwa Cristiano Ronaldo ambaye anashika nafasi ya pili kwa kuingiza pauni milioni 39.7 mwaka 2014, hii ikiwa ni kwa mujibu wa toleo jibya la jarida France Football.

Cristiano Ronaldo promotes TAG Heuer while driving a              McLaren P1 supercar in Madrid 

Nyota mwingine wa Barcelona, Neymar amekaa nafasi ya tatu kwa kutia mkononi pauni milioni 26.8 akifuatiwa na Thiago Silva (£20.2m) huku Robin van Persie ambaye anakuwa ndiye mchezaji tajiri zaidi katika Premier League, akiwa kwenye nafasi ya tano kwa kuingiza pauni  milioni 18.8.

Gareth Bale wa Real Madrid anafuatia kwa pauni milioni 17.5 na nyuma yake yupo nahodha wa Manchester United Wayne Rooney  mwenye pauni milioni 16.5.

Manchester United striker Robin van Persie is the              highest earning Premier League player on the list

Wanaokamilisha Top Ten ni Zlatan Ibrahimovic, Sergio Aguero na Robert Lewandowski lakini wakiwa wanafuatiwa kwa karibu na Eden Hazard na Yaya Toure (wote-kila mmoja £14.7m), Angel di Maria na Radamel Falcao ambao kila mmoja amejikusanyia £13.6m.

1. Lionel Messi £47.8m

2. Cristiano Ronaldo £39.7m

3. Neymar £26.8m

4. Thiago Silva £20.2m

5. Robin van Persie £18.8m

6. Gareth Bale £17.5m

7. Wayne Rooney £16.5m

8. Zlatan Ibrahimovic £15.8m

9. Sergio Aguero £15.6m

10. Robert Lewandowski £14.8m



Comments