WAKALI WAO WAFICHUA RASMI SETI YAO MPYA YA VYOMBO VIPYA VYA KISASA …tupia macho picha 14



WAKALI WAO WAFICHUA RASMI SETI YAO MPYA YA VYOMBO VIPYA VYA KISASA …tupia macho picha 14
WAKALI WAO WAFICHUA RASMI SETI YAO MPYA YA VYOMBO VIPYA            VYA KISASA …tupia macho picha 14

Kundi la Wakali Wao Modern Taradance chini yake Thabit Abdul "Mkombozi" Jumatatu mchana walifichua rasmi vyombo vyao vipya kabisa vyenye thamani ya mamilioni.

Tukio hilo lilifanyika kwenye kambi yao Mchili Pub Kinondoni  na kushuhudiwa na wadau kadhaa wa muziki.

Thabit Abdul ambaye ndiye mmiliki wa kundi hilo akaiambia Saluti5 kuwa vyombo hivyo vimegharimu milioni 24.

"Nashukuru sana, mtu mwenye moyo wa kunisaidia amejitoa muhanga na kuniwezesha kupata vyombo vipya kabisa, huu ni ukombozi mkubwa kwa kundi letu," alisema Thabit.

Thabit Abdul amewataka wapenzi wa Wakali Wao kukaa mkao wa kula kwani kuna mambo makubwa zaidi yanakuja. "Huu ni mwanzo tu, mambo mengi makubwa yanakuja."

Tazama baadhi ya picha zilizopigwa na kamera ya Saluti5 Jumatatu mchana, achana na zile zilizosambazwa na bendi hiyo kupitia Facebook. Mzigo kamili ni huu hapa.

 Hii ni Mixer mpya kabisa
 Chombo cha kuweka manjonjo (effects) kwenye magitaa
 Thabit Abdul (katikati) akijadili jambo na mtaalam wa 'sound' bwana Kiroboto (kulia)
 Tabasamu la ushindi
 Kushoto ni Mzee Sharif mwenyekiti wa Wakali Wao na kulia ni Barafu wa Bongo Movie ambaye ndiye mshauri wa bendi
 Thabit Abdul akifuatilia majaribio ya vyombo
 Spika mpya za Wakali Wao
 Spika kutoka Fidek
 Thabit Abdul akipozi kwenye moja ya vyombo vipya
 Hii ni rake ikiwa imebeba booster mbili, equalizer na crossover 
 Snake cable
 Chombo cha kudhibiti umeme (stabilizer)
 Taswira ya baadhi ya spika za Wakali Wao
Moja ya spika za bass


Comments