TOTTENHAM CHUPUCHUPU KWA WEST HAM …Harry Kane dakika ya 95


TOTTENHAM CHUPUCHUPU KWA WEST HAM …Harry Kane dakika ya 95

Harry Kane scored with the last kick of the game as                Tottenham fought back from two goals down to draw with                West Ham

Tottenham imenusurika na kipigo cha nyumbani baada ya kulazimisha sare ya 2-2 dhidi ya West Ham kwenye mchezo mkali wa Premier League.

Hadi dakika ya 81, West Ham walikuwa mbele kwa bao 2-0 kufuatia magoli ya Cheikhou Kouyate dakika ya 22 na Diafra Sakho (dakika ya 62) na ilionekana wazi kuwa Tottenham wanadondosha pointi tatu.

Lloris can't keep out Sakho's shot even though the              Frenchman was standing at his near post 

Beki wa pembeni Danny Rose akapunguza bao moja zikiwa zimesalia dakika 9 na kuamsha ari ya Tottenham.

Danny Rose strikes to pull one back for Tottenham with              10 minutes remaining in the match in north London 

Dakika tisini za kawaida zikaisha West Ham wakiwa mbele lakini dakika ya mwisho ya muda wa majeruhi (90+5) kiungo wa West Ham anayeichezea klabu hiyo kwa mkopo Alex Songo akamdondosha Harry Kane ndani ya 18 na kuwa penalti.

Alex Song brings down Kane in the final minute of the              game to give away a penalty at White Hart Lane

Harry Kane akapiga mkwaju huo wa penalti lakini kipa Adrian akapangua kabla mpira haujarejea tena kwa Kane na kufunga kirahisi bao la kusawazisha.

Kane takes the subsequent spot-kick but Adrian guesses              right and saves the initial shot 

Tottenham (4-2-3-1): Lloris 7; Walker 5.5, Dier  5, Vertonghen 5.5, Rose 6.5; Mason 5 (Chadli 80, 6), Bentaleb 5.5, Townsend 5 (Soldado 60, 5.5), Dembele 4.5 (Eirksen 46, 6), Lamela 5.5; Kane 7.

West Ham (4-3-3): Adrian 5; Jenkinson 6, Tomkins 6, Reid 6, Cresswell 6.5; Song 6, Noble 7 (Cole 68, 5 [Collins 87, 5.5]), Kouyate 7; Valencia 6 (Jarvis 74, 5.5), Sakho 6.5, Downing 6, Sakho 6.5.



Comments