Tanzania yaahidi kuwachinja wakenya leo



Tanzania yaahidi kuwachinja wakenya leo

??????????

BAADA ya timu ya Taifa ya Tanzania ya mpira wa ufukweni kuibuka na ushindi wa 5-3 dhidi ya Kenya katika mechi ya kwanza iliyopigwa wiki iliyopita huko mjini mombasa leo timu hizo zitashuka dimbani kucheza mchezo wa marudiano.

Mechi hiyo ambayo itachezwa leo
Kuanzia majira ya saa kumi jioni pale escape one itaamua ni timu gani itafuzu hatua inayofuata huku timu ya Tanzania ikiwa na nafasi kubwa ya kusonga mbele.

Wachezaji wa timu ya taifa ya Tanzania wamesema kuwa wamejipaga vizuri kuelekea mchezo huo na watafuzu hatua inayofuata ambayo watakutana na timu ya taifa ya Misri



Comments