SUAREZ APELEKA KILIO MANCHESTER CITY, BARCELONA YAPIGILIA 2-1 ...Messi akosa Penalti


SUAREZ APELEKA KILIO MANCHESTER CITY, BARCELONA YAPIGILIA 2-1 ...Messi akosa Penalti

Suarez, who scored only once in six games against City              as a Liverpool player, was on song on his return to England

Mshambuliaji wa zamani wa Liverpool Luis Suarez amerejea kwenye ardhi ya England kwa kishindo baada ya kufunga magoli yote mawili ya Barcelona kwenye ushindi wa 2-1 dhidi ya Manchester City katika mchezo mtamu wa Ligi ya Mabingwa.

Katika mechi hiyo iliyopigwa kwenye uwanja wa Etihad, Suarez alifunga katika dakika ya 16 na 30 na kuifanya Barcelona ipate faida ya magoli mawili ya ugenini.

Suarez celebrates the crucial first away goal after              finishing emphatically past Joe Hart, as Kompany looks              despondent on his knees

City itakuwa na kibarua kigumu cha kushinda kwenye dimba la Camp Nou licha Aguero kupunguza bao moja dakika ya 69.

Aguero celebrates with James Milner after scoring what              could turn out to be a vital goal in the context of the tie              with 20 minutes to go

Gael Clichy akalimwa kadi nyekundu dakika ya 74 baada kuonyeshwa kadi njano kwa mara ya pili huku Lionel Messi akipoteza penalti dakika ya 90 baada ya kipa Joe Hart kupangua kwaju huo wa miguu 12.

Manchester City: Hart, Zabaleta, Kompany, Demichelis, Clichy, Nasri (Fernandinho 61 mins), Milner, Fernando, Silva (Sagna 78), Dzeko (Bony 68), Aguero. 

Barcelona: Ter Stegen, Alves (Adriano 75), Pique, Mascherano, Jordi Alba, Rakitic (Mathieu 71), Busquets, Iniesta, Messi, Suarez, Neymar (Pedro 80).



Comments