MONACO YAIFYATUA ARSENAL 3-1 EMIRATES, WENGER ALAUMU ‘DEFENCE’ YAKE … Bayer Leverkusen yaichapa Atletico Madrid 1-0



MONACO YAIFYATUA ARSENAL 3-1 EMIRATES, WENGER ALAUMU 'DEFENCE' YAKE … Bayer Leverkusen yaichapa Atletico Madrid 1-0

Arsenal look dejected following the opener, and worse              was to come for Arsene Wenger's side, who were off the boil              all night

Arsenal ina mlima mrefu wa kupanda kama kweli inataka kupenya hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa barani Ulaya.

Hiyo ni baada ya kukubali kipigo cha bao 3-1 kwenye uwanja wake wa nyumbani (Emirates) kutoka kwa Monaco ya Ufaransa.

Hadi mapumziko Monaco ilikuwa mbele 1-0 kwa goli lililofungwa na Geoffrey Kondogbia katika dakika ya 38.

Kondogbia, who has frequently been linked with a move              to Arsenal, wheels away after his opening strike silenced              the Emirates

Geoffrey Kondogbia lets fly and his shot takes a wicked              deflection off Per Mertesacker's chest to wrongfoot David              Ospina

Shuti la Kondogbia likambabatiza Per Mertesacker  na kumpoteza maboya kipa David Ospina kabla mpira haujatinga wavuni.

Katika kipindi cha kwanza Arsenal haikufanikiwa kupiga hata shuti moja lililolenga goli

Dimitar Berbatov akarejea vizuri kwenye ardhi ya England baada ya kuifungia Monaco bao la pili iliopotimu dakika ya 53.

The former Spurs, Manchester United and Fulham striker              enjoyed his second half strike which put the game beyond              Arsenal

Mshambuliaji huyo wa zamani wa Spurs, Manchester United na Fulham alifunga bao hilo baada ya shambulizi la kushtukiza huku akiwa amezongwa na wachezaji watatu wa Arsenal.

Dimitar Berbatov rolled back the years with a glorious              finish after Anthony Martial hit Arsenal on the break with a              classic counter-attack

Mchezaji aliyetokea benchi Alex Oxlade-Chamberlain akaifungia Arsenal bao pekee katika dakika za mareruhi (90+1) na kurejesha matumani kwa wenyejeji.

Substitute Alex Oxlade-Chamberlain struck a sublime              effort deep in injury time which appeared to give the              Gunners a glimmer of hope

Lakini Arsenal ikafanya makosa katika sekunde za mwisho kabisa za mchezo (90+4) kwa kuacha lango wazi huku wachezaji wengi wakienda mbele kutafuta bao la kusawazisha na kutoa mwanya kwa Yannick Ferreira-Carrasco kuifungia Monaco goli la tatu.

But that was extinguished after Yannick              Ferreira-Carrasco punished more defensive laxity to restore              Monaco's two-goal cushion

Kocha Arsene Wenger ameishutumu vikali safu yake ya ulinzi na kukiri kuwa haikucheza vizuri.

Goli la tatu ndilo lililomkera zaidi Wenger: "Ukiwa 2-1 ukingoni kabisa mwa mwa mchezo unaacha vipi eneo lako la ulinzi wazi?" alihoji kocha huyo wa Arsenal.

Hata hivyo Wenger amesema ingawa wana mlima mrefu wa kupanda, lakini bado hawajakata tama ya kusonga mbele.

Arsenal 4-2-3-1: Ospina 7, Bellerin 4.5, Mertesacker 4.5, Koscielny 5, Gibbs 5, Coquelin 4.5 (Oxlade-Chamberlain 68, 7), Cazorla 5 (Rosicky 82), Sanchez 6, Ozil 4.5, Welbeck 5, Giroud 4 (Walcott 60, 6). Subs not used: Szczesny, Gabriel, Monreal, Chambers.

Monaco 4-1-4-1: Subasic 7, Toure 7.5, Wallace Santos 8.5, Abdennour 8, Echiejile 7.5, Dirar (Kurzawa 82), Kondogbia 8, Fabinho 7, Joao Moutinho 9, Martial 8 (Bernardo Silva 84), Berbatov 8 (Ferreira-Carrasco 76, 8). Subs not used: Stekelenburg, Matheus Carvalho, Alain Traore, Diallo.

Katika mchezo mwingine wa Ligi ya Mabingwa Bayer Leverkusen ikiwa nyumbani iliifunga Atletico Madrid 1-0 kupitia kwa Hakan Calhanoglu.



Comments