MAPACHA WATATU WALIPOPIGA SHOW YA KISOMI MLIMANI CITY MBELE YA MAPROFESA WA UDSM



MAPACHA WATATU WALIPOPIGA SHOW YA KISOMI MLIMANI CITY MBELE YA MAPROFESA WA UDSM
MAPACHA WATATU WALIPOPIGA SHOW YA KISOMI MLIMANI CITY            MBELE YA MAPROFESA WA UDSM

Ijumaa iliyopita katika kuadhimisha mwaka mpya kwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) pale Mlimani City kulikuwa na burudani moja iliyoacha gumzo la aina yake.

Burudani hiyo ilitoka kwa bendi ya Mapacha Watatu ambao ndio walikuwa watoa burudani pekee katika tukio hilo.

Mapacha wakatoa burudani ya kufa mtu iliyowaacha hoi waalikwa wakiwemo wahadhiri na wafanyakazi wote wa UDSM pamoja na viongozi wa kitaifa waliowahi kupata elimu yao katika chuo hicho.

Bendi hiyo chini ya Jose Mara na Khalid Chokoraa, ilitumbuiza kwa nyakati tofauti tofauti kuanzia saa 9 alasiri hadi saa 4 za usiku.

Moja ya vivutia kutoka kwa Mapacha ilikuwa ni namna walivyoweza kupiga muziki wa kila kona ya dunia achilia mbali nyimbo zao wenyewe.

Zifuatazo ni baadhi ya picha za Mapacha Watatu katika sherehe hizo.

 Meneja Khamis Dacota (kushoto) akipozi na Jose Mara
 Mapacha Watatu jukwaani
 Ni burudani ya kufa mtu
 Ni full kujiachia 
 Ukumbi mzima umesimama kucheza goma la Mapacha Watatu
Bata kidogo! Khalid Chokoraa, Khamis Dacota na Aristide Rubeya

 

 



Comments