MANCHESTER UNITED YAFUFUKA, YAIZIMA SUNDERLAND …Rooney moto chini



MANCHESTER UNITED YAFUFUKA, YAIZIMA SUNDERLAND …Rooney moto chini

Manchester United imerejesha makali yake kwenye Ligi Kuu ya England baada ya kuifunga Sunderland 2-0 katika mchezo mkali uliopigwa Old Trafford.

Alikuwa ni mshambuliaji Wayne Rooney aliyewapa raha mashabiki wa United baada ya kufunga magoli yote mawili.

Hata hivyo United ilibidi isubiri hadi dakika ya 66 pale Rooney alipofunga kwa mkwaju wa penalti baada ya John O'shea kumchezea faulo Radamel Falcao.

Mwamuzi Roger East akafanya kituko kwa kumpa kadi nyekundu beki Wes Brown badala ya Jonh O'shea aliyecheza faulo hiyo.

Referee Roger East wrongly sends off Sunderland              defender Wes Brown after John O'Shea conceded a penalty

Dakika ya 84 Rooney akafunga bao la pili kwa kichwa na kuzima matumaini ya Sunderland kusawazisha.

The England captain doubled his tally by heading into              an empty net to lift his side to third place in the Premier              League 

Manchester United: De Gea; Valencia, Smalling, Evans, Rojo, Blind; Herrera, Young, Di Maria (Januzaj); Rooney (Mata), Falcao (Fellaini)

Sunderland: Pantilimon; Reveillere, van Aanholt, Brown, O'Shea (c); Cattermole, Larsson, Gomez, Johnson (Fletcher); Wickham (Fletcher), Defoe (Fletcher).



Comments