CHELSEA YAVUTWA SHATI …ARSENAL YATAKATA, MANCHESTER CITY YAUA 5-0


CHELSEA YAVUTWA SHATI …ARSENAL YATAKATA, MANCHESTER CITY YAUA 5-0

An incensed Matic pushes the Burnley player to the              floor following his woeful challenge on Saturday 

Vinara wa ligi kuu Chelsea, wakicheza kwao Stamford Bridge, wametoka Sare 1-1 na Burnley ambayo inapigana isishushwe daraja.

Chelsea walitangulia kufunga kwa bao la Branislav Ivanovic la dakika ya 14 lakini wakawa pungufu katika dakika ya 70 pale Nemanja Matic alipopewa kadi  nyekundu alipolipizia rafu toka kwa Ashley Barnes. Burnley walisawazisha kwa bao la kichwa la Ben Mee kufuatia kona ya dakika ya 81.

Arsenal wakiwa ugenini walipata ushindi wa bao 2-1 walipoichapa Crystal Palace na kutwaa nafasi ya 3 kwa kuishusha Man United nafasi ya 4 mabao yakifugwa na Santi Carzola kwa mkwaju wa penati na Giroud.

Bao pekee la Palace lilifungwa dakika ya 90 na Glenn Murray.

Manchester City imepunguza pengo kwa Chelsea hadi kufikia pointi tano baada ya kuifumua Newcastle 5-0 kwa magoli ya Sergio Aguero, Samir Nasri , Edin Dzeko  na David Silva aliyefunga magoli mawili.

Sergio Aguero scored a second-minute penalty to give              Manchester City the lead against Newcastle United at the              Etihad Stadium

Matokeo ya mechi zote zilizochezwa Jumapili ni:

Aston Villa 1 - 2 Stoke City

Chelsea 1 - 1 Burnley

Crystal Palace 1 - 2 Arsenal

Hull City 2 - 1 Queens Park Rangers

Sunderland 0 - 0 West Bromwich Albion

Swansea City 2 - 1 Manchester United

Manchester City 5 - 0 Newcastle United



Comments