AZAM FC YATUPWA NJE KLABU BINGWA AFRIKA (3-2) …EL MERREIKH YASHINDA 3-0 NYUMBANI



AZAM FC YATUPWA NJE KLABU BINGWA AFRIKA (3-2) …EL MERREIKH YASHINDA 3-0 NYUMBANI
AZAM FC YATUPWA NJE KLABU BINGWA AFRIKA (3-2) …EL            MERREIKH YASHINDA 3-0 NYUMBANI

Mabingwa wa Tanzania Bara, Azam FC wametupwa nje ya michuano ya klabu bingwa Afika baada ya kukubali kichapo cha 3-0 ugenini dhidi ya El Merreikh ya Sudan.

Azam imeshindwa kulinda ushindi wake wa 2-0 ilioupata katika mchezo wa kwanza uliofanyika Azam Complex jijini Dar es Salam na hivyo kuaga kwa jumla ya bao 3-2.

El Merreikh walifunga bao moja katika kipindi cha huku mawili yakija ukingoni mwa kipindi cha pili.

Mchezo huo umechezwa Jumamosi jijini Khartoum kwenye uwanja wa Merreikh kuanzia saa 2 za usiku kwa saa za Afrika Mashariki.
Kwa mujibu wa matangazo ya moja kwa moja ya Radio Uhuru, waamuzi kutoka Zambia walionekana wazi kuwabeba wenyeji.



Comments