TORRES APELEKA KILIO BERNEBE, REAL MADRID YATEMESHWA NA ATLETICO MADRID TAJI LA KWANZA …sasa Atletico kukutana na Barcelona nusu fainali


TORRES APELEKA KILIO BERNEBE, REAL MADRID YATEMESHWA NA ATLETICO MADRID TAJI LA KWANZA …sasa Atletico kukutana na Barcelona nusu fainali

Torres enjoyed a slice of good fortune as goalkeeper              Keylor Navas deflected the ball into the net for his second              goal

Fernando Torres anafungua ukurusa mpya katika historia yake baada ya kufunga bao lake la kwanza ndani Santiago Bernabeu, kitu ambacho hakawahi kufanya hapo kabla akiwa na timu yoyote ile.

Hiyo ilikuwa katika mechi kali marudiano ya kombe la Copa del Rey kati ya Atletico Madrid na Real Madrid iliyokuwa uwanja wa nyumbani ikipambana kufuta bao 2-0 ilizofungwa na Atletico kwenye mchezo wa kwanza wiki iliyopita.

Fernando Torres celebrates opening the scoring for              Atletico Madrid after just 49 seconds at the Bernabeu

Torres akatupia bao mbili na kuisadia Atletico Madrid kulazimisha sare ya 2-2 na kusonga mbele kwa jumla ya bao 4-2, hii ikimaanisha kuwa Real Madrid wametema taji la kwanza miongoni mwa mataji manne waliyoshinda mwaka jana.

Hii ni awamu ya pili kwa Torres kuichezea Atletico Madrid timu yake ya tangu utotoni kabla hajaenda Liverpool, Chelsea na AC Milan.

Katika awamu yake ya kwanza ya kuitumikia Atletico, Torres hakuwahi kuifunga Real Madrid hata bao moja, jambo lilifanya mashabiki waliofurika Santiago Bernabeu Alhamisi usiku wamkejeli wakiamini kuwa hana madhara yoyote kwao.

Lakini ilimchukua Torres sekunde 49 tu kuwajibu mashabiki hao baada ya kuifungia Atletico bao la kwanza lililowafanya Real Madrid wawe na mlima mrefu wa kupanda.

Real defender Sergio Ramos (right) rises to head home              the first equaliser on Thursday night

Ramos celebrates after scoring in the first-half of the              Madrid derby on Thursday night

Beki Sergio Ramos  akasawazisha kwa kichwa dakika ya 20, kabla ya Torres ambaye alifunga bao moja tu katika miezi yake minne aliyoichezea AC Milan, hajaifungia Atletico goli la pili dakika ya kwanza tu baada ya kuanza kwa kipindi cha pili.

Mchezaji bora wa dunia Cristiano Ronaldo akaifungia Real Madrid bao la pili dakika ya 54. Safari ya Real Madrid kutetea kombe hilo la Mfalme ikakomea hapo.
Kwa matokeo hayo, Atletico sasa itakutana na Barcelona katika hatua ya nusu fainali.



Comments