STURRIDGE AREJEA UWANJANI



STURRIDGE AREJEA UWANJANI
DanielSturridge
MSHAMBULIAJI wa Liverpool,  Daniel Sturridge anaweza kurudi uwanjani kesho kuivaa Chelsea katika mechi ya marudiano ya nusu fainali ya kombe la ligi itayopigwa uwanja wa Stamford Bridge ikitokea katika majeruhi ya muda mrefu, amesema kocha Brendan Rodgers.
Nyota huyo wa zamani wa Chelsea, Sturridge ambaye aliifungia Liverpool magoli 25 kwenye mashindano yote msimu uliopita hajaingia uwanjani tangu mwezi wa nane mwaka jana kufuatia kupata majeruhi.
Sturridge alikwenda Marekani wakati wa Krismas kupata matibabu na aliporudi alianza mazoezi,na Rodgers anatumaini kumuona mshambulizi huyo wa England akiwakabilia Chelsea.
"Amefanya mazoezi vizuri, sana jana (Sturridge) na ameonekana kuimarika", Rodgers amewaambia waandishi wa habari.


Comments