Mwanzoni mwa mwezi Disemba mwaka jana, waimbaji nyota wa Jahazi Modern Taarab, Khadija Yussuf na Fatma Mohamed "Mcharuko" walikaribishwa studio za Pili Pili FM ya mjini Mombasa na kufanya mahojiano mafupi.
Fatma Mcharuko au Fatma Nyoro kama anavyojiita sasa hivi pamoja na Khadija Yussuf walifanya mahojiano na mtangazaji Aisha Abushiry maarufu kama Mamaa Madikoko kupitia kipindi cha kila siku cha Chachandu za Taarab.
Mamaa Madikodiko ameiambia Saluti5 kuwa kama kuna siku ambayo alipokea meseji nyingi kwenye kipindi chake basi siku aliyowahiji Khadija na Mcharuko ni moja siku zilizopata meseji kibao kutoka kwa wasikilizaji wao.
Mcharuko na Khadija walikuwa Mombasa kwaajili ya tamasha kubwa Usiku wa Mirindimo lililofanyika mjini humo.
Khadija Yussuf (kushoto) na Fatma Mcharuko (kulia) wakiwa na Mamaa Madikidiko
Khadija Yussuf, Mamaa Madikidiko na Fatma Mcharuko
Khadija Yussuf, Mamaa Madikidiko na Fatma Mcharuko katika picha ya pamoja
Khadija Yussuf akiwa katikati ya mahojiano
Mamaa Madikoko akisoma meseji za wasikilizaji





Comments
Post a Comment