PSG YAONA MWEZI, YASHINDA 4-2 … ushindi wa kwanza baada ya mechi nne


PSG YAONA MWEZI, YASHINDA 4-2 … ushindi wa kwanza baada ya mechi nne

Former Chelsea defender David Luiz is congratulated by              Italian midfielder Marco Verratti and Brazilian midfielder              Lucas Moura

Paris Saint-Germain (PSG) imeichapa Evian 4-2 kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya Ufaransa na kusogea hadi nafasi ya tatu kwenye msimamo wa Ligue 1.

Ulikuwa ni ushindi wa kufa na kupona kwa PSG ambayo inaendelea kubaki nyuma kwa pointi nne kwa vinara wa ligi hiyo Olympique Lyonnais iliyoichapa RC Lens 2-0 Jumamosi.

Huu ni ushindi wa kwanza kwa PSG ndani ya mechi zake nne za mwisho, shukurani kubwa ziwaendee Pastore na Cavani waliofunga magoli ya ushindi.

Kiungo wa kimataifa wa Ufaransa Cedric Barbosa alifunga bao tamu la kuongoza kwa Evian dakika ya 14 lakini beki wa zamani wa Chelsea David Luiz akaisawazishia PSG dakika 15 baadae.

Brazilian duo Luiz and Thiago Silva run towards the PSG              home fans to celebrate the former Chelsea defender's goal

Marco Verratti akapatia PSG bao la pili dakika ya 38, goli lililodumu hadi dakika ya 63 wakati Gregory van der Wiel alipojifunga na kufanya mambo yawe 2-2.

Kiungo wa Kiargentina Javier Pastore akawafungia mabingwa watetezi goli la tatu kunako dakika ya 74 huku Edinson Cavani akihitimisha ushindi kwa kupachika bao la nne dakika moja kabla ya mpira kumalizika.

PSG's Argentinian midfielder Javier Pastore (middle)              celebrates with teammates Verratti (left) and Brazilian              defender Maxwell

Uruguayan striker Edison Cavani celebrates scoring              PSG's fourth goal of the game against Evian in Ligue One



Comments