Bendi maarufu ya muziki wa          dansi barani Ulaya, Ngoma Africa band aka FFU-Ughaibuni, ambayo          pia hujulikana kama  viumbe wa ajabu Anunnaki Alien. Bendi hii          inayoongozwa na mwanamuziki Ebrahim Makunja aka kamanda Ras          Makunja  imejikuta ipo katika hali ya kukosa usingizi tena baada          ya kutakiwa kutumbuiza maonyesho zaidi katika msimu ujao wa joto          (Summer).  Watayarishaji wa maonyesho makubwa ya nje barani          Ulaya wanashinikizwa na washabiki wao lazima waipandishe          jukwaani Ngoma Africa Band kutokana na mdundo wao Bongo dansi,          mapromota hao baada kuwekwa roho juu na washabiki wao, nao          wamedhamiria kuwapambanisha washabiki hao na bendi maarufu Ngoma          Africa band yenye makao yake nchini Ujerumani. Habari za uhakika          zimetonya kuwa bendi hiyo imekubali kuenda kutumbuiza katika          nchi za Latvia na Austria na maonyesho mengine katika msimu wa          joto, pia taarifa zinasema kuwa hali hiyo ya tabia za washabiki          kushinikiza maonyesho inaifanya bendi ya Ngoma Africa band kuwa          katika mzunguko wa maonyesho makubwa na wanamuziki kukosa muda          wa kupumzika.Lakini hakuna ubishi kuwa kamanda Ras Makunja na          kikosi chake wanauwezo wa aina yake wa kuwamudu washabiki wao          kule barani Ulaya. FFU-ughaibuni pia wanasikika online at www.ngoma-africa.com
Comments
Post a Comment