LIVERPOOL YAANZA KUCHANGANYA, YAIPA ASTON VILLA 2-0 …kocha azomewa


LIVERPOOL YAANZA KUCHANGANYA, YAIPA ASTON VILLA 2-0 …kocha azomewa

Fabio Borini has his shot to score the opening goal              against a hapless Aston Villa early on during the Premier              League match

Liverpool imeenaza kuwa tishio kwa timu zinanyatia nafasi ya kucheza Ligi ya Mabingwa barani Ulaya baada ya kupata ushindi mwingine muhimu dhidi ya Aston Villa.

Ikicheza ugenini, Liverpool ikatandaza soka safi na kuvuna ushindi wa bao 2-0 huku kocha wa Aston Villa, Paul Lambert akizidi kupata shinikizo kwa mashabiki wa timu hiyo.

The ball goes into the back of the net against Aston              Villa as Liverpool take the lead in the 24th minute in the              Premier League

Wakati Aston Villa ikienda mapumziko ikiwa nyuma kwa bao la dakika ya 24 lililofungwa na Fabio Borini, mashabiki wenyeji waliojazana kwenye uwanja wa Villa Park, walimzomea kocha huyo kuonyesha kukerwa kwao na ukame wa ushindi.

Hadi sasa Aston Villa hajapata ushindi katika jumla ya masaa 8 na dakika 42 katika mechi mbali mbali ilizoshiriki.

Rickie Lambert aliyetokea benchi ndiye aliyekuwa mwiba zaidi kwa Aston Villa baada ya kupachika goli la pili dakika ya 79.

Lambert runs away in celebration after doubling              Liverpool's lead with a little more than 10 minutes              remaining at Villa Park

Aston Villa: Guzan 7.5, Hutton 6,5, Okore 6, Baker 6, Cissokho 5, Sanchez 7, Westwood 5 (Gil 5, 59), Delph 6.5, Cleverley 4 (Weimann 6, 59), Agbonlahor 4, Benteke 6

Liverpool: Mignolet 7.5, Can 8, Skrtel 7.5, Sakho 6.5, Markovic 6.5, Moreno 6.5 (Enrique 6, 71), Lucas 7.5, Henderson 8, Sterling 6.5 (Ibe 85), Coutinho 8.5, Borini 7 (Lambert 7, 71)



Comments