JUAN CUADRADO ABISHA HODI CHELSEA, ANDRE SCHURRLE SAFARINI KUREJEA BUNDESLIGA


JUAN CUADRADO ABISHA HODI CHELSEA, ANDRE SCHURRLE SAFARINI KUREJEA BUNDESLIGA
JUAN CUADRADO ABISHA HODI CHELSEA, ANDRE SCHURRLE            SAFARINI KUREJEA BUNDESLIGA

Chelsea imekubali kumuuza Andre Schurrle ili kutunisha mfuko wa kumsainisha mshambuliaji Juan Cuadrado (pichani juu kushoto) kutoka Fiorentina.

Hatua ya Chelsea kumsajili Cuadrado, 26, nyota wa Colombia inaweza kukamilika muda mfupi ujao na kuwahi mechi ya kufa na kupona dhidi ya Manchester City wikiendi hii.

Cuadrado could be registered in time to face                Manchester City at Stamford Bridge on Saturday eveningĀ 

Chelsea inataka pauni milioni 30 kwa Schurrle, 24, na Wolfsburg ya Ujerumani inaongoza mbio za kumrejesha nyumbani mshambuliaji huyo, Borussia Dortmund nayo pia inamtaka.

Jose Mourinho si mshambiki wa mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Ujerumani, lakini anajua thamani yake sokoni. Mshindi huyo wa Kombe la Dunia anataka kurejea nyumbani.

Chelsea haina haraka ya kumuuza  Schurrle (pichani chini) lakini imekuwa ikitamfuta mbadala wake ambapo Cuadrado na Douglas Costa ndio walengwa wakuu.

Andre Schurrle appears to have played his last game for              Chelsea after they agreed to cash in on the forward

Kama dili la Schurrle litakamilika basi Chelsea itazitumia pesa hizo kumsajili Cuadrado ambaye ana kipengele cha pauni milioni 26.8 kwa klabu inayotaka kuvunja mkataba wake.



Comments