JOSE MOURINHO AANZISHA ‘NONGWA’ NA FA



JOSE MOURINHO AANZISHA 'NONGWA' NA FA
252020E900000578-0-image-m-47_1422407807575
Jose Mourinho na  Diego Costa wakizungumza wakati wa mechi dhidi ya Liverpool
Jose Mourinho amenuna baada ya chama cha soka England, FA kusema kinamtoza faini Diego Costa kwa kuonesha mchezo usiokuwa wa kiungwana.
Mourinho ameichukia FA na anaamini mfungaji wake anayeongoza kufumania nyavu ametolewa kama mbuzi wa kafara kufuatia kumchezea vibaya beki wa Liverpool, Emre Can.
Kocha huyo wa Chelsea ambaye amewahi kutozwa faini na FA alitakiwa kuwa na mkutano na waandishi wa habari kesho ijumaa kuelekea mechi ngumu dhidi ya Manchester City jumamosi, lakini ameufuta.
 
Diego Costa appears to stamp on Emre Can's right leg                during a feisty Capital One Cup clash with Liverpool
 
Diego Costa alionekana kumkanyaga mguu wa kulia  Emre Can kwenye mechi ya nusu fainali ya Capital One dhidi ya  Liverpool
Costa could now face a three-game ban after being                    charged by the FA for his stamp on Can
Costa anaweza kufungiwa mechi tatu baada ya kutozwa faini na FA kutokana na kitendo hicho alichomfanyia Can.
Klabu ya Chelsea imefuta ratiba ya mkutano na waandishi wa habari na hatawathubutu hata kumtuma kocha msaidizi, Steve Holland kuzungumza na vyombo vya habari.
Imethibitishwa kuwa kikao cha nidhamu cha FA kitakachokaa kesho kitamuadhibu Costa.
Licha ya Costa kukataa kosa lake, mshambuliaji huyo wa Chelsea anatarajia kufungiwa mechi tatu kuanzia ya jumamosi dhidi ya Man City.


Comments