Jordan              Henderson (wa pili kulia) na Diego Costa (kulia) pia              walirushiana maneno walipokuwa uwanjani
          JORDAN              Henderson na Diego Costa wameripotiwa kuwa na ugomvi              walipokutana nje ya vyumba vya kubadilishia nguo baada ya              mechi ya kwanza ya nusu fainali ya kombe la ligi iliyopigwa              jumanne iliyopita kwenye uwanja wa Anfield baina ya              Liverpool na Chelsea.
          Wawili              hao waliwakiana vikali na kutaka kupigana, lakini              waliamuliwa na wahudumu wa vyumba vya kubadilishia nguo.
          Inaaminika              kwamba hawakurushiana ngumi, lakini wachezaji hao walisukuma              kwa hasira na kurushiana maneno.
        Henderson              alionekana kumuonesha kitu na Costa akiwa amemtumbulia macho
        
Comments
Post a Comment