TIMU za Tunisia na DR Congo            zimefanikiwa kutinga hatua ya Robo Fainali Afcon 2015 kutoka            Kundi B huku Cape Verde na Zambia zikiaga mashindano hayo            yanayoendelea huko Equitorial Guinea.
                Timu hizo zimetinga hatua hiyo baada            ya kutoka sare ya bao 1-1 kwenye mchezo wao wa mwisho            uliopigwa leo huku Zambia na Cape Verde wakitoka suluhu na            kuondolewa.
        Zambia na Tunisia wameungana na            Congo pamoja na Equitorial Guinea waliokata tiketi zao za robo            fainali jana kutoka Kundi A.
        Tunisia wamemaliza wakiwa vinara wa            Kundi B kwa kuwa na pointi 5 huku DR Congo wakiwa nafasi ya            pili na pointi zao 3.
        Kesho Senegar watamenyana na Algeria            huku Ghana wakikwaana na Afrika Kusini katika kusaka tiketi ya            kutinga robo fainali kutoka Kundi C.
        
Comments
Post a Comment