Kiungo wa Partizan Belgrade, Danilo Pantic amethibitisha kuwa amekamilisha taratibu zote za kujiunga na Chelsea.
Vinara wa Premier League wameipiku Juventus ambayo nayo ilikuwa inamwania kwa udi na vumba kinda huyo wa miaka 18, nyota wa timu ya taifa ya Serbia kwa vijana wenye umri chini ya miaka 19.
Pantic anajiunga na Chelsea kwa ada ya pauni milioni 1.25 na imebainika kuwa atapelekwa kukipiga kwa mkopo kwa klabu ya Vitesse Arnhem hadi mwisho wa msimu huu.
Comments
Post a Comment