TONY PULIS AKATAA KUWA KOCHA MPYA WA NEWCASTLE …ahofia kupangiwa list na mmiliki wa timu


TONY PULIS AKATAA KUWA KOCHA MPYA WA NEWCASTLE …ahofia kupangiwa list na mmiliki wa timu

Pulis has been out of work since leaving Crystal                Palace before the start of the Premier League season

Tony Pulis amekataa nafasi ya kuwa kocha mpya wa Newcastle United, akihofia kuwa kikosi cha kwanza kitakuwa kikipangwa na kamati.

Kocha huyo wa zamani wa Stoke na Crystal Palace amewaambia washauri wake kuachana na mazungumzo na Newcastle baada ya kuingia hofu kuwa mmiliki mtata wa klabu hiyo, Mike Ashley na skauti mkuu wa kusaka wachezaji Graham Carr watakuwa wakiingilia upangaji wa timu.

Ashley na Carr walisimamia usajili wa wachezaji, hali ambayo Alan Pardew alikubaliana nayo. Lakini inaaminika ndiyo sababu iliyomfanya atimke na kujiunga na Crystal Palace.

Tony Pulis amekuwa hana kazi tangu alipoiacha Crystal Palace muda mfupi kabla Ligi Kuu haijaanza.



Comments