Na Bertha Lumala
          Simba SC imepata pigo katika kambi yake Visiwani Zanzibra baada          ya mshambuliaji wake hatari Elias Maguli kuumia.
Baada ya kuichapa Yanga SC mabao 2-0 katika mechi ya 'Mtani          Jembe 2′ kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam Desemba 13,          kikosi cha wekundu hao wa Msimbazi klikwenda Zanzibar jana          mchana kuiwekea kambi Timu ya Kagera Sugar FC kabala ya mechi          yao inayofuata,
          
          Simba SC itakuwa na kibarua kigumu mbele ya kikosi cha Mganda          Jackson Mayanja cha Kagera Sugar FC watakapokutana katika mechi          ya raundi ya nane ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL)          msimu huu itakayochezwa Uwanja wa Taifa Ijumaa.
Mratibu wa kambi ya Simba SC visiwani humo Abdul Mshangama amesema Maguli ameuamia kifundo cha mguu wakati wa mazoezi.
"Tunaendelea vizuri na mazoezi ingawa mshambuliaji wetu Maguli ameumia mguu. Wataalam wetu wa tiba wanamuangalia lakini taarifa za awali zinaonesha hatakuwa nje ya uwanja kwa muda mrefu," amesema.
Comments
Post a Comment