Alan              Irvine yuko kiti moto katika kazi yake West Brom
          Tim              Sherwood anapigiwa upatu zaidi wa kurithi mikoba ya Alan              Irvine aliyetimuliwa kazi katika klabu ya West Bromwich              Albion na uteuzi wake unaweza kutangazwa mwishoni mwa wiki              hii.
          Kocha              huyo wa zamani wa Tottenham Hotspur alibaki kidogo kupata              kazi Hawthorns majira ya kiangazi mwaka jana, lakini              mazungumzo yalivunjika kutokana na maslahi.
          Sherwood              anatamani kuwatumia wasaidizi wake Les Ferdinand na Chris              Ramsey.
          Kama              atapata kazi hiyo, makocha wasaidizi wa timu hiyo Keith              Downing na Rob Kelly watabaki kwenye sintofahamu.
        Kocha              wa zamani wa Tottenham Hotspur, Tim Sherwood anapewa nafasi              kubwa ya kupata kazi West Brom
        
Comments
Post a Comment