Gareth              Bale akiwa na makombe aliyoshinda tangu ajiunga na Real              Madrid majira ya kiangazi mwaka 2013 ambayo ni (kutoka              kushoto kwenda kulia) Kombe la klabu bingwa ya Dunia, Ligi              ya mabingwa Ulaya, Kombe la Hispania na UEFA Super Cup.
          MATUMAINI              ya Manchester United kuinasa saini ya Gareth Bale yamegonga              mwamba kufuatia Real Madrid kuda kamwe haitamuuza              mshambuliaji huyo.
          Louis              van Gaal amekuwa akihusishwa na kufanya uhamisho mkubwa kwa              Bale utakaogharimu paundi milioni 120 ambaye alisajiliwa              majira ya kiangazi mwaka 2013 na miamba ya Hispania, Real              Madrid kwa ada ya uhamisho ya paundi milioni 86 akitokea              Tottenham Hospurs.
          Ripoti              kutoka Hispania zinaeleza kuwa United walikuwa tayari              kumsajili Bale, lakini Rais wa Real,  Florentino Perez              amedai nyota huyo mwenye miaka 25 hauzwi kwa bei yoyote ile.
        Perez            alisema: 'Sidhani kama Real Madrid itaenda bila Bale. Hatuwezi            kusikiliza ofa yoyote bila kujali ni kiasi gani".
        "Huyu            ni mchezaji wa kipekee ambaye ametufaidisha mengi na ni muhimu            sana kwa hatima ya baadaye ya klabu".
        
Comments
Post a Comment