PAUL NONGA:MVUA IMETUNYIMA USHINDI MKUBWA


PAUL NONGA:MVUA IMETUNYIMA USHINDI MKUBWA
Picture 029
Mshambuliaji  nyota wa Mbeya City Fc Paul Nonga amesema mvua kubwa iliyonyesha  masaa mawili kabla ya mchezo wa ligi kuu ya soka Tanzania Bara  baina ya timu yake na Ndanda Fc  uliochezwa kwenye  uwanja wa Sokoine jijini Mbeya  imesababisha kukosekana kwa ushindi  wa idadi kubwa ya mabao  waliokuwa wamepanga kuupata.
Akizungumza mapema leo Nonga  aliyefanikiwa kupachika mabao 6 kwenye ligi msimu uliopita alisema  kuwa yeye na wachezaji wenzake walikuwa wamejiandaa kushinda mchezo huo kwa idadi kubwa   ya magoli lakini mvua iliyonyesha iliwafanya kushindwa kucheza vizuri kufuatia utelezi uliokuwepo uwanjani hapo.
"Mchezo ulikuwa mzuri, lakini mvua imetufanya  kushindwa kupata mabao mengi kutokana na kuwepo utelezi mwingi uwanjani, tulijiandaa kushinda kwa idadi kubwa  lakini pia tunashukuru kwa  ushindi tuliopta kwasababu tumeongeza poiti tatu muhimu tulizokuwa tunazihitaji zaidi" alisema Nonga
Katika mchezo huo uliohudhuriwa na mashabiki kutoka sehemu mbalimbali za jiji la Mbeya City ilifanikiwa kuibuka na ushindi wa bao 1-0 lililofungwa na Deus Kaseke katika dakika ya 5 ya mchezo.
DSC_0801
Fredy Cosmas  wa Mbeya City Fc (kulia) akipiga mpira mbele ya  Zabron Raymond wa Ndanda Fc ya Mtwara.


Comments