Katibu mkuu wa YANGA Dr Tiboroha            akizungumza na waandishi wa habari,pembeni yake ni Jerry Muro            mkuu wa idara ya mawasiliano ya klabu hiyo 
Katibu mkuu mpya wa YANGA Jonas Tibohora aahidi makubwa kwenye          klabu hiyo, Katibu mkuu huyo mpya leo amezungumza na waandishi          wa habari kwa mara ya kwanza tangu aingie madarakani.
          DrJonas Tibohora amesema anataka kuiongoza Yanga kujiendesha          kiuchumi, katika mpango wake huo anataka kuanza kutengeneza          kikosi imara cha ushindani ikiwa ni pamoja na kutengeneza mifumo          bora ya soka la vijana klabuni hapo
          Lengo kubwa la kuwekeza kwenye timu za vijana ni kujalibu          kupunguza ghalama za kununua wachezaji kutoka nje,pia amesema          sasa ni muda wa klabu hiyo kunufaika na nembo ya klabu hiyo          kibiashara.
Comments
Post a Comment