MARTIN ODEGAARD KINDA ANAYEPASUA VICHWA VYA MANCHESTER UNITED, CITY, LIVERPOOL NA BAYERN MUNICH


MARTIN ODEGAARD KINDA ANAYEPASUA VICHWA VYA MANCHESTER UNITED, CITY, LIVERPOOL NA BAYERN MUNICH

Martin Odegaard is set to visit Manchester United and              Manchester City this week as the Stromsgodset youngster              chooses which club to join. Bayern Munich and Liverpool are              also interested in the 16-year-old star

Kinda mchawi wa soka kutoka Norway, Martin Odegaard anatarajiwa kuzitembelea Manchester United na Manchester City wiki ijayo katika kile kinachoonekana kama ni njia yake ya kuchagua timu ya kujiunga nayo.

 

Dogo huyo mwenye umri wa miaka 16 mwenye uwezo wa hali ya juu wa kutandaza soka, anataka kuzitembelea klabu zote kubwa zinazosaka saini yake.

Odegaard has already been capped three times for              Norway, including this appearance against Bulgaria 

Martin Odegaard anayecheza nafasi ya kiungo, tayari alishatembelea mazoezi ya Manchester United mapema msimu huu, lakini anataka kufanya mazoezi na kikosi cha kwanza cha timu hiyo.

City ilishaanza kufanya maongezi na klabu ya kinda huyo, Stromsgodset lakini timu hiyo ya Norway imesema mchezaji huyo yuko huru kuamua wapi pa kwenda.

Bayern Munich inaamini wana nafasi nzuri ya kumsani kinda huyo, lakini inajua wazi kuwa Odegaard alifurahia maisha yake ya siku mbili ndani ya Liverpool, klabu anayoishabikia tangu utotoni mwake.



Comments