KIPA HUGO LLORIS WA TOTTENHAM AINYIMA USHINDI MANCHESTER UNITED


KIPA HUGO LLORIS WA TOTTENHAM AINYIMA USHINDI MANCHESTER UNITED

Lloris pulls off another stunning one-handed save to                deny Ashley Young, whose shot was curling dangerously                towards the far corner

Imekuwa ni vigumu kwa msimu huu, kumfunika kipa wa Manchester United David De Gea, lakini Jumapili hii mlinda mlango wa Tottenham Hugo Lloris amefanya hivyo baada ya kuwa shujaa wa kupangua mashuti ya washambuliaji wa United.

Katika dakika ya 45 za mwanzo Hugo Lloris akapangua michomo ya kadhaa ya Falcao na Robin van Persie ambayo ni wazi kuwa bila umahiri wake, basi Tottenham ingekwenda mapumziko ikiwa imeshabugizwa zaidi ya mabao mawili.

Phil Jones looks on from the floor as his header is              palmed over the line by Hugo Lloris, but the goal was              disallowed for offside

Dakika ya 34 Lloris alifanya kazi ya ziada kuodoa hatari iliyosukumizwa na Falcao, kabla nafasi nzuri zaidi ya kipindi hicho cha kwanza haijamdondokea Van Persie.

Michael Carrick alimtengea mpira mzuri Van Persie, akiwa amebaki yeye na Lloris ndani ya kisanduku cha sita, badala ya kufunga akaamua kuremba, Lloris akamdhibiti kwa mguu wake mithili ya sentahafu.

The France captain Lloris stood up well to deny Van              Persie, who should really have scored with the best chance              of the first 45 minutes

Muda mfupi baadae Lloris akacheza vizuri krosi ya Ashley Young, kabla ya kupangua mkajwa wa Juan Mata.

Kipindi cha pili kilikuwa cha mashambulizi ya kupokezana ingawa ni Tottenham iliyokuwa nyumbani ndiyo iliyokuwa hatari zaidi lakini hadi mwisho wa mchezo si United wala Tottenham iliyopata bao.

Tottenham: Lloris 8, Chiriches 6, Fazio 6, Vertonghen 6, Davies  6, Stambouli 5.5, Mason 5.5, Townsend 6 (Dembele 79 mins), Eriksen 5.5, Chadli 5 (Lamela 79), Kane 6. 

Manchester Utd: De Gea 6, Jones 6.5, McNair 5 (Shaw 75), Evans 6 (Smalling 72), Carrick 7.5, Valencia 5.5 (Rafael 46), Mata 7.5, Rooney 6.5, Young 7, van Persie 5, Falcao 4. 



Comments