Meneja uhusiano wa                Airtel Tanzania,Jackson Mmbando (kulia)  na Meneja masoko                wa Airtel Tanzania, Bi. Aneth Muga (kushoto) wakiwa kwenye                picha ya pamoja na washiriki wa Airtel Trace Music Stars                leo mara baada ya washiriki hao kuongea na waandishi wa                habari kwaajili ya kuomba wananchi kuwapigia kura. 
                Meneja uhusiano wa                Airtel Tanzania,Jackson Mmbando akiongea na waandishi wa                habari (hawapo pichani) wakati alipotangaza washiriki                waliongia nafasi ya kumi bora katika mashindano ya Airtel                Trace Music Stars kwa wiki hii. Kulia ni Aneth Muga Meneja                Masoko wa Airtel Tanzania anaesimamia mashindano hayo ya                Airte Trace Music Stars. Hafla ya kutangaza washiriki hao                wa 10 bora aimefanyika makao makuu ya Airtel jijini dar es                salaam leo.
                Meneja Masoko wa Airtel                Tanzania,Bi. Aneth Muga akielezea jinsi ya kupiga KURA kwa                washiriki waliofanikiwa kuingia 10 bora ya mashindano ya                Airte Trace Music Stars. Kulia ni meneja uhusiano wa                Airtel Jackson Mmbando katika hafla ya kuwatangaza                washiriki hao iliyofanyika ofisi za Airtel makao makuu                morocco Dar es salaam leo.
                Mshiriki wa Airtel Trace                na moja kati ya 10 bora Karen Gardner akionyeshanamba yake                ya ushiriki 55100107 kwa watanzania kumpigia kura. 
                Mshiriki wa Airtel Trace                na moja kati ya 10 bora Christopher kiwele akionyesha                namba yake ya ushiriki 55100050 kwa watanzania kumpigia                kura. 
                Mshiriki wa Airtel Trace                na moja kati ya 10 bora Jesca charles akiwa pamoja na                meneja uhusiano wa Airtel Jackson Mmbanod , akionyesha                namba yake ya ushiriki 55100135 kwa watanzania kumpigia                kura. 
                Mshiriki wa Airtel Trace                na moja kati ya 10 bora John Chambasi akionyesha namba                yake ya ushiriki 55100005 kwa watanzania kumpigia kura. 
                Mshiriki wa Airtel Trace                na moja kati ya 10 bora Vanessa Galinoma akiimba na                kuonyesha namba yake ya ushiriki 55100232 kwa watanzania                kumpigia kura. 
        Kampuni ya simu za                mkononi ya Airtel leo imetangaza washiriki walioingia kumi                bora wiki hii katika mashindano ya Airtel Trace Music                Stars yenye lengo la kuvumbua na kusaka vipaji vya                wanamuziki chipukizi nchini na Afrika kwa ujumla
        Shindano hilo                lililozinduliwa mwanzoni mwa mwenzi wa Kumi, linaendelea                kuwapatia watanzania na wapenzi wa muziki nafasi ya                kushiriki kwa kupiga namba 0901002233 na kurekodi wimbo                 na kuutuma kisha wimbo huo kutasminiwa na jopo la majaji                na kufudhu kuingia katika hatua ya kupigiwa kura .
        Akiongea na waandishi wa                habari Meneja Masoko wa Airtel Bi Anneth Muga alisema"                tunafurahi kuona jinsi gani watanzania wanavyoitikia na                kushiriki katika shindano hilo ambapo mpaka sasa limedumu                kwa takribani mienzi miwili na nusu. Leo hii tunao                wanamuziki chipukizi ambao wameweza kuibuka kuwa katika                kumi bora ya wiki hii na tunapenda kuwatangazia jamii,                wapenzi wa muziki ili muweze kuwapigia kura na waweze                kuendelea kufanya vizuri katika mashindano haya.
        Napenda kuchukua fulsa                hii kuwakumbusha watanzania kwa Mshindi wa Airtel Trace                Music Stars atapatikana kwa vigezo viwili vikubwa  kwanza                ni kwa uwezo wake wa kuimba  na pili kutokana na wingi wa                kura ,  hivyo tumeona ni vyema sasa kuwaleta kwenu ili                muweze kuwawezesha kutimiza ndoto zao  waendelee kwa                kuwapigia kura ilie kufanya vizuri kwenye mashindano haya
        Kwa upande wake Meneja                Uhusiano wa Airtel Jackson Mmbando alisema " kwa sasa tuko                kwenye hatua muhimu sana ya kuwawezesha washiriki hawa                kuendelea mbele kwa kupiga kura, kura yako ndio                inahitajika sasa ni rahisi sana  unaweza kupiga kura kwa                kupiga namba 0901002233 Kisha ukachagua lugha  na kufata                maelekezo, ili kuupigia kura wimbo au mshiriki ni lazima                uwe na kodi ya namba yake ya ushiriki hakikisha una kodi                namba ya mshiriki unayetaka kuumpia kura wakati wote wa                kupiga kura kisha utapata maelekezo ya kuingiza kodi hiyo                na baada ya kuingiaza utasikia wimbo wa mwimbaji na kuamua                kumpigia kura. Njia ya pili ni kwakuandika ujumbe wenye                kodi namba ya ushiriki na kisha kuituma kwenye namba 15594                na tayari utakuwa umepiga kura yako.
        Tutaendelea kuwajulisha                washiriki watakao ingia kumi bora kila wiki na ili kupata                habari hizi kwa urahisi basi tembelea facebook page yetu                ya Airtel Tanzania na upata kuona picha za washiriki                mbalimbali, namba zao za ushiriki na kusikiliza nyimbo zao                kupitia simu yako ya mkononi. Natoa wito kwa watanzania                kuendelea kushiriki kwenye mashindano haya kwa kujisajili                na kurekodi na kwa kupigia kura washiriki ili tupate                mwakilishi bora atakayekwenda kutuwakilisha kwenye                mashindano ya Airtel Music Trace Afrika yatakayoshirikisha                nchi 17 za Afrika hapo mwaka kesho " aliongeza mmbando
        Akiongea wakati wa                maojiano na waandishi wa habari mmoja kati ya washiriki                kumi bora wa wiki hii Jesca Charles alisema" najisikia                furaha sana kuingia katika kumi bora ya wiki hii, naomba                watanzania wanipigia kura kwa wingi ili nisishuke                nieendelee kufanya vizuri. Napenda sana kuimba na ndoto                yangu ni kuwa mwimbaji wa kimataifa na mwimbaji nae vutiwa                nae ni Beyonce natumaini siku moja ntafikia na kuwa                mwimbaji nyota kama Beyonce"
        Washiriki Walioingia                kumi bora wiki hii ni pamoja na Christopher kihwele namba                ya ushiriki 55100050, karen Gardner 55100107, Mwinyimkuu                Hussein 55100048, John chambasi 55100005, Vanessa Galinoma                55100232, Jesca Charles 55100135, Anne Mkisi 55100004
        Mashindano ya Airtel                Trace yatafikia kilele mwanzo mwa mwaka kesho ambapo                mshindi wa Airtel Trace Afrika atajishindia zawadi kabambe                ikiwemo, kurekodi na kusambaziwa nyimbo zake chini ya                studio kubwa ulimwenguni pamoja na  safari kwenda nchini                marekani na kupata mafunzo ya kimuziki na Nguli wa Muziki                wa Amerika Akon
        







Comments
Post a Comment