AC MILAN YAIFANYIA KITU MBAYA REAL MADRID …yaichapa 4-2 na kutibua rekodi yao ya mechi 22


AC MILAN YAIFANYIA KITU MBAYA REAL MADRID …yaichapa 4-2 na kutibua rekodi yao ya mechi 22

Stephan El Shaarawy scored twice for AC Milan as they              beat La Liga leaders Real Madrid 4-2 in a friendly on              Tuesday evening

Real Madrid imetibua rekodi yake ya kutofungwa tangu mwezi Septemba baada ya kukubali kipigo cha 4-2 kutoka kwa AC Milan katika mchezo wa kirafiki uliochezwa Dubai Jumanne jioni.

Stephan El Shaarawy alifunga mara mbili katika dakika ya 31 na 49 huku Menez akifunga dakika ya 24 na Pazzini akimalizia kwa bao la dakika ya 73.

Cristiano Ronaldo got himself on the scoresheet in the              first half to halve the deficit before half time

Ronaldo aliifungia Real Madrid bao muhimu dakika ya 35 likiwa ni la kusawazisha kabla ya AC Milan haijacharuka na kuangusha karamu ya magoli huku Karim Benzema akiipunguzia aibu timu yake kwa kufunga bao la pili kwa njia ya penalti dakika ya 84.

Kocha wa Real Madrid Carlo Ancelotti aliingia mapumziko ya majira ya barafu akiwa na rekodi ya kushinda mechi 22 mfululizo lakini makamanda wake Cristiano Ronaldo na wenzake wakafichwa na AC Milan inayosota nafasi ya saba kwenye msimamo wa Serie A.

AC Milan captain Riccardo Montolivo holds aloft the              Dubai Football Challenge trophy after beating Real Madrid              4-2

Kwa ushindi huo, AC Milan wakatwaa kombe maalum la Dubai Football Challenge.



Comments