Mlinzi wa kati wa klabu ya Liverpool, ndugu wa kiungo Yaya          Toure, Kolo Toure amesema kuwa meneja wa majogoo hao wa Anfield          Brendan Rodgers anamkumbusha enzi za kocha wake wa zamani Arsene          Wenger na hivyo anaamini ataubadili msimu mbaya klabuni hapo.
          Ikumbukwe kuwa, klabu hiyo la liverpool imekuwa na mwenendo          mbaya siku za karibuni kufuatia kupoteza mechi nne mfululizo          kabla ya kuambulia sare kunako michuano ya klabu bingwa ulaya          dhidi ya Ludogorets ya Bulgaria jumatano usiku.
          Liverpool inashika nafasi ya 12 katika ligi ya uingereza pamoja          na kuwa miongoni mwa timu zilizofanya vizuri msimu ulopita,          lakini Kolo Toure bado anaamini ndiye meneja sahihi anayepaswa          kuendelea kuinoa miamba hiyo na kuikwamua pale ilipo. Nyota huyo          ni miongoni mwa wachezaji walounda kikosi cha Arsenal          kilichomaliza msimu bila kupoteza 2003-04
          Mchezaji huyo pia alipata kushinda taji la ligi kuu ya uingereza          msimu wa 2012 akiwa na klabu cha Manchester City lakini bado          anaamini meneja wake huyo wa Liverpool, Brendan Rodgers          anashabihiana na Arsene wenger. "namwona wenger ndani yake kwani          ana akili" alieleza Liverpool Echo:
          "Anajua namna ya kuongea na wachezaji, na namna ya kuwatumia          ipasavyo, nina uhakika atalithibitisha hilo mara atapoikwamua          klabu katika kipindi hiki kigumu" "kama Arsene daima amekuwepo          mazoezini ili kuboresha mambo, hata mbinu zao zinafanana kwani          daima amekuwa akituhimiza kucheza soka la pasi na kumiliki"
          
          Toure (33) ameendelea kusisitiza kuwa klabu ya Liverpool          inapaswa kuendela kumuunga mkono Rodgers, wakatio akiendela          kuboresha mambo kunako michuano ya klabu bingwa ulaya.          "tunapaswa kuendelea naye maana yeye ni mmoja wa makocha bora          katika ligi ya uingereza".
          "siku zote kama meneja wa timu unahitaji muda, ni kama msimu          uliopita ulivyokuwa wa kushangaza pamoja na kwamba mambo ni          magumu kwa sasa ila bado naamini amefanya kazi kubwa na hivyo          kama timu tunampenda, michuano ya ulaya ni migumu ndo sababu          ukitizama hata vilabu kama Manchester City unapata funzo".
          "Daima amekuwa akijitoa kwa kila kitu, tizama namna alivyofanya          mambo makubwa katika kipindi kifupi. Alipokuja hapa hali ilikua          mbaya lakini alibadilisha kila kiyu, naamini hata safari hii          itafanikiwa. Alimalizia nyota huyo. 
Comments
Post a Comment