Na Bertha Lumala, Dar es Salaam
          UONGOZI wa Stand United inmayoshiririki kwa mara ya kwanza Ligi          Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) msimu huu, umesafiri kutoka          usukumani mjini Shinyanga hadi maeneo ya Jangwani jijini hapa          kuzungumza na uongozi wa Yanga SC ili uwasajili Said Bahanunzi,          Omega Seme na Hamis Thabit kipindi hiki cha usajili wa dirisha          dogo.
          Mkurugenzi wa Ufundi wa Stand United, Muhibu Kanu ameuambia          mtandao huu jijini hapa leo kuwa ameamua kuja kuteta na uongozi          wa Yanga SC ili aruhusiwe kuwanasa wachezaji hao kuimarisha          kikosi chao kilichop[o nfasi ya 10 katika msimamo wa VPL kikiwa          na pointi tisa sawa na Mgambo walioko nafasi ya tisa, Polisi          Morogoro (8) na Simba (7).
          Mashabiki wa Stand United            wakiingia kwenye Uwanja wa CCM Kambarage mjini Shinyanga kabla            ya kuanza kwa mechi ya timu yao iliyopita dhidi ya Yanga.            Stand ililala 3-0
          "Kuna baadhi ya wachezaji wetu tutakosa huduma zao kwa sababu          wanatakiwa na timu za ndani na nje ya nchi. Musa Said anatakiwa          na Kaizer Chief ya Ligi Kuu ya Afrika Kusini, Heri Halifu          anatakiwa na Mbeya City," kiongozi huyo amesema.
          "Kuna wengine wanatakiwa na JKT Ruvu, hivyo tunaona tuje Yanga          kusaka wachezaji watakaotuongezea nguvu. Tayari tumezungumza na          uongozi wa Yanga, wametuambia tuandike barua na tumefanya hivyo          maana pesa ipo."
          Aidha, Mkurugenzi huyo amesema wanamnyatia pia mchezaji Jamil          Mchaulu 'Balotelli' wa Azam FC na kwamba tayari wameshaundikia          barua uongozi wa wanalambalamba juu ya suala hilo.
          Amesema wachezaji wote hao wanawataka kwa mkopo.
          Katibu Mkuu wa Yanga, Beno Njovu na Meneja wa Timu ya Azam,          Jemedari Said wamekiri kupokea maombi ya Stand United.
          "Masuala yote ya wachezaji yako chini ya kocha mkuu (Marcio)          Maximo. Atakapowasili nchini Jumatano tutamweleza, kama ataona          inafaa kuwaachia wachezaji hao tutaruhusu," amesema Njovu.
          Bahanunzi, aliyeibuka mfungaji bora wa Kombe la Kagame mwaka          juzi katika msimu wake wa kwanza Yanga SC akitokea Azam FC,          amekuwa akisugua benchi katika kikosi hicho cha Jangwani, hivyo          kuonekana kama hana lolote.
Comments
Post a Comment