MASHABIKI WA KLABU YA LIVERPOOL WALIVYOFIKISHA UJUMBE WAO KUPINGA KUPANDA KWA BEI ZA TIKETI ZA KLABU YAO

Mashabiki wa klabu ya              Liverpool siku ya jana waliutumia mwanya walioupata kwenye              mchezo wa ligi dhidi ya timu ya Stoke City kwa kupeperusha              bango kubwa lilionesha kutoridhika kwao kwa kitendo cha              kupandishiwa bei ya tiketi kwenye michezo ya klabu hiyo.
                      Mashabiki hao walilionesha                bango hilo lililoonesha namna ambavyo bei ya tiketi kwa                klabu yao imekua ikipanda kwa ghafla tangu mwaka wa 1990                mpaka kufikia hivi sasa.
            Kwenye bango hilo                mashabiki hao walionesha kuwa bei ya tiketi ya                kuwashuhudia majogoo hao wa Anfield ilikua paundi 4 mnamo                mwaka 1990, ambayo ilipanda mpaka kufikia kiasi cha paundi                24 mnamo mwaka 2000 na sasa ghalama hiyo imepanda mpaka                kufikia kiasi cha paundi 43 mnamo mwaka 2010 mpaka sasa.
           
Comments
Post a Comment